Halloween party ideas 2015
Showing posts with label Ulaya. Show all posts


Lionel Messi ameifungia  hat-trick timu yake ya Barcelona  dhidi ya Granada katika ushindi wa 4 - 0 na kuiwezesha Barcelona kukaa kileleni mwa msimamo mwa ligi kuu Hispania  La Liga .

Messi aliweza kufunga mara mbili ndani ya dakika 14 na baadae alifunga tena dakika ya 58, na goli la nne limefungwa na Neymar dakika ya 83.


Zinedine Zidane Akiongea na Waandishi wa Habari
Zinedine Zidane akiwa kama kocha mpya wa Real Madrid baada ya kutimuliwa kwa aliyekuwa kocha wa timu hiyo Rafa Benitez . Akizungumza na waandishi wa habari, ametoa msimamo wake juu ya uwezekano wa kuuzwa kwa Cristiano Ronaldo kwamba hawana wazo hilo kwa sasa.

Kocha Mpya Zinedine Zidane akiwa katika majukumu yake mapya kama kocha.




Mshambuliaji wa Everton, Romelu Lukaku akiifungia timu yake katika ushindi wa 2-1 dhidi ya Manchester City mechi ya kwanza ya Nusu Fainali ya Kombe la Ligi, maarufu kama Capital One Cup Uwanja wa Goodison Park usiku wa jana. Bao lingine la Everton limefungwa na Ramiro Funes Mori, wakati la City lilifungwa na Jesus Navas 


Bosi wa Timu Rayo Vallecano Paco Jemez amesema Timu yake ilifedheheshwa na kudhalilishwa ilipobamizwa Mabao 10-2 wiki hii kwenye Mechi ya La Liga Uwanjani Santiago Bernabeu.

Amesema kipigo hicho kimeaibisha Soka la Spain na kuipotezea imani.Hiyo ilikuwa ni mara ya kwanza kwa Real Madrid kufunga Bao 10 kwenye Mechi ya La Liga tangu Mwaka 1960 walipoifunga Elche 11-2.
Akijibu madai ya Jimenez, Kocha wa Real, Rafa Benitez, alisema: "Kuna mechi nyingi hata sisi tulionewa, hatukunufaika. Sikusema lolote wakati huo na sitasema kitu sasa.”
Ligi kuu ya Hispania kwa sasa inaenda Mapumziko ya Siku 10 kwa ajili ya sikukuu ya Krismasi na Mwaka mpya.


Ligi kuu ya soka ya England imendelea tena hapo jana kwa michezo miwili ,ambapo Watford waliwaalika Liverpool na matokeo ni kwamba Watford imechomoza na ushindi mnono wa mabao 3-0 ambayo yamefungwa na wachezaji Nathan Aki pamoja na Idion Ighalo akifunga mabao 2 , likiwa ni bao la 12 kwa mchezaji huyo katika msimu huu.

Katika mchezo mwingine swansea dhidi ya West Ham ni kwamba mchez huo ulimalizika kwa timu hizo kutoshana nguvu kufuatia sare ya bila kufungana (0-0) .
Ligi hiyo itaendelea tena kwa mchezo mmoja ambapo Arsenal watakuwa nyumbani Emirate wakiwakaribisha Manchester City.
Real Madrid imeiadhibu Rayo kwa mabao 10-2 La Liga.


Klabu ya soka ya Real Madrid iliifanikiwa kuichapa Timu ya Rayo Vallecano Bao 10-2 katika Mechi ya ligi kuu ya ispania maarufu kama (La Liga ) .

Madrid walianza kufunga mabao kupitia Danilo na Rayo Vallecano wakasawazisha na kuongeza bao na kuongoza ikiwa ni bao 2-1.
Katika ushindi wa mabao hayo 10-2 -mbali na mchezaji Danilo mabao mengine ya madridi yalifungwa na wachezaji Gareth Bale mabao manne (4) , Cristiano Ronaldo mabao mawili (2), Karim Benzema mabao matatu (3), huku mabao ya Rayo Vallecano yakifungwa na Antonio Amaya Pamoja na Jozabed.
Ushindi huu umewabakisha Real Madrid katika Nafasi ya 3 wakiwa Pointi 2 nyuma ya Vinara Barcelona na Atletico Madrid .


 Louis van Gaal akalia Kuti Kavu Baada ya  Manchester Unite kupoteza tena mchezo dhidi ya Norwich City
wakiwa nyumbani Old Trafford . Hii ni mfululizo wa matokeo mabaya yanayoiandama Manchester United kwa sasa baada ya Kutolewa katika kugombea ubingwa wa ulaya(UEFA Champion League).

Magoli ya Norwich City yamefungwa na Cameron Jerome na Alex Tettey, na Manchester walifunga kupitia kwa Anthony Martial.

Powered by Blogger.

Powered by themekiller.com