Halloween party ideas 2015


Somalia imetangaza kuvunja uhusiano wa kidiplomasia na Iran ikiituhumu kwa kuingilia masuala ya ndani ya Somalia.

Serikali ya Somalia imewapa maafisa wote wa ubalozi wa Iran mjini Mogadishu muda wa saa 72 (siku tatu) wawe wameondoka nchini humo.
Uamuzi huo umechukuliwa baada ya mkutano wa baraza la mawaziri wa Somalia.

“Hatua hii imechukuliwa baada ya kutathminiwa kwa kina na kutokana na hatua ya Jamhuri ya Iran kuendelea kuingilia masuala ya ndani ya Somalia,” taarifa kutoka wizara ya mashauri ya kigeni ya Somalia imesema.

"Jamhuri ya Somalia inaitaka Jamhuri ya Kiislamu ya Iran kuheshimu uhuru wa mataifa yote kwa mujibu wa sheria za kimataifa, Mkataba wa Vienna kuhusu Uhusiano wa Kidiplomasia wa mwaka 1961 na tamaduni za uhusiano wa kidiplomasia.

Post a Comment

Powered by Blogger.

Powered by themekiller.com